
Tutagharamiaje Upunguzaji wa Umasikini?
Hatuna hakika tunahitaji fedha kiasi gani na kiasi gani cha fedha kitakuwepo katika
siku zijazo. Hata hivyo ni wazi kuwa hatutakuwa na fedha za kutosha na zile ndogo
tulizonazo itabidi tuzitumie kwa uangalifu mkubwa.
Hatutaweza kujua kwa hakika ni fedha kiasi gani zitapatikana hasa kwa ajili ya
kupunguza umasikini mpaka mipango yote mingine iwe imekamilika.
Njia za Mapato kwa ajili ya Upunguzaji Umaskini
 | Kiasi fulani cha fedha kitatokana na bajeti ya Serikali lakini hatutaweza kujua kiasi
cha fedha kitakavyokuwa hadi mfumo wa kodi utakapoboreshwa. · |
 | Kiasi cha fedha kitatoka kwa wafadhili, lakini kiasi hicho hakiwezi kujulikana katika
muda mfupi na muda mrefu · |
 | Serikali itatumia fedha zake kupata fedha zaidi kwa kutoa mikopo na michango kwa watu wa
kawaida na wafanyabiashara ambao wana mawazo mazuri na miradi mizuri · |
 | Serikali inaweza kukopa fedha kuziba pengo |
Kwa kuzingatia hali hii ya mashaka, na umuhimu wa kuwa na uchumi thabiti, matarajio
yaliyowekwa kwa miaka mitatu ijayo ni kuwa jumla ya bajeti ya matumizi itaongezeka toka
asilimia 15.5 hadi 17-18% ya mapato yote ya serikali. Kati ya fedha hizo asilimia 70%
itatoka serikalini na asilimia 30% itatoka kwa wafadhili kama misaada au mikopo. Kama
Mageuzi ya Serikali yatafaulu basi Tanzania itatimiza masharti ya mpango nafuu yaliyowekwa
kwa ajili ya nchi zenye madeni makubwa (HIPC) hadi kufikia katikati ya mwaka 2001.
Shughuli nyingi za upunguzaji wa umasikini zitafanywa na Serikali za Mitaa. Ufafanuzi
wa shughuli hizi utafanywa katika Programu ya Mageuzi ya Serikali za Mitaa (LGRP)
yanayoendelea.
Kipaumbele katika Matumizi
Katika majibu ya watu waliyotoa wakati wa kutayarisha Mkakati wa Kupunguza Umasikini
(PRSP), serikali imeamua kuwa matendo muhimu katika upunguzaji wa umasikini yanapaswa
kuwa; matengenezo na uimarishaji wa huduma za sekta muhimu na sehemu inyohusika. Matendo
hayo ni kama yafuatayo:
| |
Shilingi Milioni |
|
|
| Elimu ( Elimu ya Msingi) |
|
| Afya (Afya ya Msingi kwa Jamii) 65970 42314 Barabara (Vijijini) |
|
| Barabara (Vijijini) |
|
| Mfumo wa Mahakama |
|
| Kilimo (Utafiti na huduma) |
|
| Maji |
|
| VIRUSI VYA UKIMWI/UKIMWI |
|
Upunguzaji wa Umasikini: Vipengele Muhimu vya Ziada
Ufutaji wa ada za Shule \
Serikali itaacha kutoza ada za shule ifikapo Julai 2001. Hii ni kwa sababu serikali
inaamini kwamba kwa kutolipa ada watoto wengi watasoma hasa watokao katika familia
masikini
Kuhimiza michango kutoka katika Jumuiya na Washika dau wengine
Jumuiya zimeshiriki kikamilifu daima katika kupunguza umasikini kwa kufanya kazi za
kujitolea kama kujenga madarasa, vituo vya afya, maji, barabara za vijijini, n.k. Serikali
itahimiza moyo huu kwa kuchangia gharama za miradi hii na kuwahamasisha wafadhili kufanya
hivyo hivyo.
Mafunzo ya Kazi
Serikali inakusudia kutumia karibu shilingi milioni 100 kila mwaka ili kuwasaidia watu
waweze kujifunza mambo yatakayowasaidia kupata kazi. Fedha hizi zitawalenga watu ambao
hasa ni masikini zaidi.

|